welcome note


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, August 29, 2011

..bukoba trip.... fantastic trip

Bukoba mkoni Kagera, huendeka kwa njia zote za usafiri, yaani majini, angani na hata kwa nchi kavu. nlibahatika kwenda huko August mwanzoni mwaka huu kwa matembezi kama mtalii ndani ya nchi yangu tena ukizingatia napenda safari hivo hata sikusita kukubali pale niliposikia juu ya safari hii.

Hapo ndo safari ilikuwa yaanza yapata mida ya saa tatu, kutokea Mwanza ndani ya MV Victoria siku ya alhamisi tarehe 04/August 2011. Hivo pembeni ni vyumba vya first class, chumba kimoja wanalala watu wawili, pale nyuma kidogo kuna mlango wa kuelekea third class.


hapo ni sehemu tu ya mji huo kwa mbali kutokea highland moja wapo ambapo kuna gud view ya ziwa na mji kwa mbali aisee pale mahala ni pazur jaman adi raha, ebu endelea ona, other views.........


kisiwa kimoja wapo ndani ya ziwa victoria huko bukoba, kisiwa hiki wanaishi wavuvi kwa asilimia kubwa


hapo ni lake view mida ya jioni hiviiii


na hapo ni sehemu ya mji wa bukoba wakati wa jioni


hapa ilikuwa jumamosi asubuhi jaman, kutokana na vinywaji vya ijumaa ilikuwa ni wakati muafaka wa kupata supu, sasa yalotokea hapo jama ndo kama uonavyo hapo juu, kwa pale hiyo ni supu tena its  tshs 7000/= per bowl only jaman, bakuli 1 lina samaki mzima na ndizi, na la pili lina kuku nusu na viazi....... aisee nlichoka mhhhh...


sasa matembezi c ndo yakaanza, ni  katika baadhi ya vijiji kama mwenyeji wangu alivopanga, kijiji cha kwanza kilikuwa Ibosa, nikawa naonyesha  mazao maaruf ya mahal hapo. Kuanzi tu ni mkahawa na kahawa zake kama inavooneka hapo juu


kama kawada, ndizi c ndo fahari ya wahaya wapatikanao Bukoba, ebu cheki zilivonona mhhh....imagine zimepikwa...yumm yumm....


ushawahi ckia mto kagera jaman?, basi hiyo ni side moja wapo ya mto huo uliopo eneo liitwalo Kyaka, mto unapatikana njian on the way to Mutukula (mpaka wa Tanzania na Uganda) na vijiji vingine vipatikanavyo barabara hiyo


ushawahi sikia kanisa lililochomwa moto na nduli Iddi Amini likiwa na waumini siku ya jumapili wakati wa vita kati ya Tanzania na Uganda? basi ndo hilo hapo juu lapatikana Kyaka na  laitwa.... jina limenitoka kidogo, atakaekumbuka aandike jina basi wandugu


huu ni mnara wa mashujaa waliopigana vita vya Kagera, ni kilometa tano tu kabla ya kufika Mutukula(mpakani mwa Tanzania na Uganda)


na hayo ndo majina ya mashujaa 


na hapo ni kuelekea kijijini Gwanja, kuna mahali panaitwa Nyakijoga, inavodaiwa eneo hilo ilionekana sura ya mama bikira Maria ndani ya maji, na hado sasa sehemu hiyo ni tajkatifu na watu wengi kutoka sehemu mbalimbali  huenda kuhiji


"karibu bukoba mwanakwetu"
huwez amin mwenyeji wa nyumba hiyo ndo alinipa beseni lotee hilo la matunda niweze kula mhhh, parachichih nusu tu, kwisha habari yangu, lilikuwa tamu yummm....yummmm. alaf nlishiba adi aibu mhh...


nice view from far kama inavoonekana wakati natokea kijijini Kashasha kuelekea kijijini Gwanja


sa we upite barabara za vijiji vya bukoba alaf usikutane na mandhari haya.....ahhh itakuwa BK feki


lenye mwanzo lina mwisho mwenzangu, J3 ndo hiyo imefika, na mrembo Mv Victoria kwa mbaaaaaaliiii kule nyuma yangu amepaki akinisubiri mi na abiria wengine muda wa saa tatu usiku arud Mwanza. 


navuta pumzi  kidogo nikiwa nakula upepo wa beach ya Bukoba


bye bye Bukoba, it was nice accomodating me all gud 4 days, i had fun and enjoy a lot for real.


sasa wandugu tujaribu tembelea miji na mikoa mbalimbali ya nchi yetu pale tunapopata nafasi, kwani ts enjoyabo and very fantastic, lets try this japo once in a year, it helps a lot guys.........

4 comments:

  1. Jamani bukoba kwetu nimepamiss vibaya ....

    it seemed you enjoyed a lot

    ReplyDelete
  2. best inaelekea ulienjoy ile mbaya...mida mingine ukitaka kwenda nishtue nami nikatoe ushamba...kumbe Bukoba pazuri eeenh

    ReplyDelete
  3. ahhh ni sana tu, bukoba na Tanzania kwa ujumla ni pazuri sana jaman

    ReplyDelete
  4. mh isijekuwa fix huogopi maji wewe?tueleze salaam zao tangu asubuhi hadi kulala au hukulala kabisa!ee bebi mambo yamekunyookea kaza buti na mwendo mdundo jitahidi spelling cheking kabla ya kupost best of luck and have fun

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...